Loading...
http://go.ad2up.com/afu.php?id=778977

BREAKING NEWS: TUNDU LISSU AZUA ZOGO ZITO MAHAKANI LEO AZIDI KUMSHAMBULIA RAIS MAGUFULI NA KUMTOLEA KAULI HIZI TATA RAIS MAGUFULI....

Tundu Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema) akiwasili mahakama ya Kisutu pamoja na wafuasi wa chama hicho
TUNDU Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki amesema, ‘namtaka dikteta uchwara mahakamani,’anaandika Faki Sosi.
Lissu ambaye ni Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni amesema hayo leo muda mfupi baada ya kutoka kusikiliza shauri lake katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam la kudaiwa kutoa kauli ya uchochezi.
“Mimi na jopo langu la mawakili tunamtaka niliyemuita diktekta uchwara aje mahakamani kuthibitisha udikitekta uchwara wake,” amesema Lissu.
Lissu amefunguliwa shitaka la uchochezi katika mahakama hiyo, kesi yake inasikilizwa na Hakimu Yohona Yongolo ambapo kwa upande wa mashitaka, unawakilishwa na Benard Kongolo, wakili wa serikali mkuu.
Lissu alijisalimisha jana 5 asubuhi katika kituo hicho cha polisi ambapo alizuiliwa kupewa dhama na kulala hadi alipofikishwa mahakamani leo.
Wafuasi na viongozi mbalimbali wa Chadema walifika mahakamani hapo akiwemo Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa chama hicho taifa; Salum Mwalim, Kaimu Katibu Mkuu Zanzibar na Benson Kigaila, Mkuu wa Operesheni wa chama hicho.
Wakili Kongolo amedai kuwa, Lissu alitenda kosa hilo tarehe 28 Juni mwaka huu katika eneo la Mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam kwa kuzungumza;
“Mamlaka ya Serikali mbovu ni ya kidiktekta uchwara inahitaji kupingwa na kila Mtanzania  kwa nguvu zote, huyu dikitekta uchwara lazima apingwe kila sehemu kama uongozi utafanywa na utawala wa kijinga nchi inaingia ndani ya giza nene.’’
Hata hivyo, Lissu amekana shitaka hilo, amedhaminiwa na wadhamini wawili waliosaini hati ya Sh.2 milioni kila mmoja na masharti ya kutosafiri nje ya nchi na kwamba, upelelezi wa kesi hiyo umekamilika. Kesi hiyo itatajwa kwa kusikilizwa tarehe 2 Agosti mwaka huu.
Upande wa utetezi kuliwakilishwa na mawakli 11 miongoni mwao ni Michael Ngolo, Peter Kibatala, John Mallya, Hekima Mwasibu, Omari Msemo, Jeremia Mutasebya na Juma Nasoro.
Nje ya Mahakama
Alipotoka nje ya mahakama Lissu alizungumza na wafuasi wa Chadema walifurika katika viwanja hivyo pamoja na waandishi wa habari ambapo amesema, “nilijua kwamba wenye busara watanyamaza baada ya mimi kutoa kauli ile juzi mahakamani hapa.
Hata hivyo, Lissu amesema kuwa, katika kituo alicholazwa ameshuhudia watu wakiteseka kutokana na kutopelekwa mahakamani kwa muda wa wiki mbili hadi mwezi mmoja na kuwa, hupewa mateso makali mpaka kusababisha wengine kuvunjwa miguu.
Mbowe amewaambia waandishi wa habari kuwa, uonevu wa utawala wa sasa unafanywa bungeni na nje ya bunge na kwamba, hawatakata tamaa ya kupigania haki.
Wakati huo huo Jeshi la Polisi limewatia mbaroni wafuasi wanne wa Chadema walikuwa wamebeba mabango yenye maneno ‘Dikitekta Uchwara nenda Burundi,’ Polisi ‘Uchwara acheni kutumika’ na ‘Lisuu Tanzania inakuhitaji

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright JAMIIYETU | Designed By BAKI NASI
Back To Top