Loading...
http://go.ad2up.com/afu.php?id=778977

Watawala chimbuko la machafuko

John Magufuli, Rais wa Tanzania akiwa na Jakaya Kikwete, Rais Mstaafu wa awamu ya nne wa Tanzania
IMEELEZWA kuwa machafuko mengi ambayo yanatokea duniani yanatokana na watawala kuminya haki kwa wanaowatawala, anaandika Dany Tibason.
Hayo yamebainishwa na Imamu mkuu wa msikiti wa Nunge,Al-Hajj Sheikh Ahmed Zuber, alipokua akitoa salamu za Eid-El Fitr katika kiwanja cha mpira cha Jamhuri mjini Dodoma.
Kiongozi amesema kutokana na watawala kushindwa kutoa haki kwa wananchi kumesababisha kuwepo kwa machafuko katika maeneo mengi duniani.
Mbali na hilo amesema watawala wengi wamekuwa na tabia za kutaka wananchi wao kujua haki zao jambo ambalo linasababisha watu wengi kunyanyaswa.
“Mafarakano mengi yanatokana na watawala kutokujua matatizo makubwa na wananchi wao huku watawaliwa wakiwa hawajui haki zao”amesema sheik Al Hajj Zuberi.
Katika hatua nyingine amesema kazi ya vita dhidi ya ufisadi inatakiwa kukemewa na kupingwa na watu wote bila kujali itikadi ya kidini wala vyama vya siasa.
Amesema licha kuwa serikali imekuwa na nia njema ya kupambana na ufidadi lakini viongozi wa dini wanakazi kubwa ya kuwaubiria waumini wao ili wawe na hofu ya Kimungu.
Kutokana na hali hiyo amewataka waumini ya dini ya kiislam kuendelea na ibada na matendo mema kama walivyokuwa wakifanya wakati wa Ramadhani.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright JAMIIYETU | Designed By BAKI NASI
Back To Top