Loading...
http://go.ad2up.com/afu.php?id=778977

BREAKING NEWS: KIMENUKA BUNGENI BUNGE LAFANYA MAAMUZI MAGUMU KUWAHI KUTOKEA BAADA YA SAKATA HILI NYETI ..

Image result for bunge tanzania

BUNGE limeukataa rasmi Mkataba wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Jumuiya ya Ulaya (EU) na ya Afrika Mashariki (EPA) na kuishauri serikali isiusaini.

Limesema kama kutakuwa na nafasi ya majadiliano, basi marekebisho makubwa yafanyike kwa maslahi ya Taifa ili kwenda sambamba na sera ya kodi na ya uchumi wa viwanda ya nchi.

Aidha, wameishauri serikali kupeleka bungeni mikataba mingine inayogusa maslahi ya Taifa, ikiwemo ya gesi, mafuta na madini ili ijadiliwe na Bunge liishauri serikali kama ilivyofanya kwa mkataba huo wa EPA ili kuisaidia nchi isiingie katika mikataba ya kinyonyaji.

Mazimio ya Bunge yalifikiwa jana, bungeni mjini hapa baada ya wabunge kuujadili mkataba huo na kisha Spika wa Bunge, Job Ndugai kuwahoji wanaoafiki usainiwe na wasioafiki. Kwa mara ya kwanza na kwa kauli moja, wabunge wa upinzani walieleza misimamo yao na vyama vyao kuwa Serikali isiusaini mkataba huo kwa kuwa hauko kwa maslahi ya nchi.

Msimamo huo ulitawala mjadala kwa pande zote ikiwemo kwa wabunge wa chama Tawala (CCM) waliochangia pamoja na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, iliyowasilisha mkataba huo bungeni juzi na ulitakiwa kujadiliwa kesho, Alhamisi lakini umejadiliwa jana kutokana na juzi Bunge kuahirishwa kufuatia msiba wa Spika Mstaafu wa Bunge la Tisa, Samuel Sitta.

“Kwa kauli moja Bunge linaishauri Serikali isisaini mkataba huu. Katika Mkutano wa Nne wa Bunge jambo hili lilikuwepo na ilionekana wabunge wapate nafasi ya kuishauri Serikali. Utakuwa na utaahira fulani mkataba huu ukasainiwa kwa jinsi ulivyo. Lo! Hapana haiwezekani,” alisema Ndugai akitoa maazimio ya Bunge baada ya kuwahoji wabunge.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright JAMIIYETU | Designed By BAKI NASI
Back To Top