Loading...
http://go.ad2up.com/afu.php?id=778977

SHUJAA LEMA ANDIKA HISTORIA HII MPYA ILIYOTUKUKA KWA TAIFA LA TANZANIA HAKIKA DAIMA SHUJAA HUISHI MILELE..

SHEIKH HUYU KIBOKO YA WOTE
Kwako Comrade G.Lema; Najua mapito unayopitia kwasasa, ni mapito makubwa sana yenye historia kubwa inayochochea hasira na kuamsha hisia Kali.

Nataka ujue na dunia ijue upo Mahabusu siyo kwasababu ya kubaka ama kuzini, upo kwasababu umekataa uonevu,umekataa kuishi ukiwa umepiga goti umekataa kuwatukuza wasiyositahili kutukuzwa, umekataa kuwapa utukufu usiyokuwa wao wala ukuu usiyositahili kwao.

Furaha yangu nipale ninapowaona wanajaribu kutisha mtu asiyeogopa mtu ambaye wakati wote amekuwa akiyaishi Yale anayonena...

Comrade Lema... najua jambo lililopo mbele yako ni jambo dogo kwako kwa aina ya siasa zako naona wanazidi kuiambia dunia na ulimwengu aina ya kamanda wanaopambana naye...

Comrade Lema... Wewe ni shujaa wetu na itabaki kuwa hivyo, unatupa somo sisi Wanasiasa wengine namna ya kuitafuta haki bila kuipigia goti, unatupa somo kubwa sana, kama tulifikiri tumefika tusahau na tuone ndiyo kwanza tumeanza Safari ya mabadiliko, Umetuamsha ya kwamba tulikuwa tumejisahau kuna wajibu tumeupuuza kipindi Fulani...

Comrade Lema.... Jina lako lipo juu ya Mlima mrefu hakuna wakufikia kileleni pale isipokuwa Jah pekee ndiyo mwenye Mkono huwo, Maono yako ni makubwa si Rahisi Mwanadamu asiye kuwa na Imani kufikiri kuwa ni imani na imani hukaa na mwenye imani...

Comrade Lema... Mara nyingi sana umekuwa ukituambia USIOGOPE nasi twasema USIOGOPE imani yetu IPO kwako...

Comrade Lema... Umekuwa ukisema ni heri ya vita inayitafuta haki na usawa kuliko amani inayopumbaza na kudhalilisha utu wa Mwanadamu, ni maneno ya kijasiri yanayoweza kutamkwa na mtu mwenye hofu ya mungu kwakuwa anajua alitendalo...

Comrade Lema... Huna mfano wa kufananishwa kwasasa kwa aina ya siasa zako za level ya juu sana, pengine ni kwasababu unaongoza jimbo lenye Wananchi wenye uelewa mkubwa sana, ndiyo maana umekuwa ukifikiri makubwa wakati wote.

Comrade Lema... Wananchi wako wa Arusha mjini wanakupenda sana kuliko mtu mwingine yoyote yule mpaka imefikia mahali wanazuia wasije mahakamani siku ya kesi zako, Ila hakimu ameliona hilo na kukemea, huu ni upendo wa wazi kutoka kwa Wananchi wako Mpaka walikuweka ndani Wanaona wivu wanaamua kutumia nguvu kuwazuia...wanatamani wangependwa wao Ila haitawezekana kwakuwa Wanawaarusha wanakuamini wewe...

Comrade Lema: kwasasa kila Mwanasiasa kijana anatamani kufanya siasa kama zako, huu ni utukufu usiyolazimishwa bali umekuja wenyewe kwa upendo...

Comrade Lema... Uimara wako,ujasiri wako unazidi kutuimarisha na kutupa nguvu na sababu za msingi za kutokukata tamaa, Watu wanasema, kama Mbunge anaswekwa ndani kwanini Mimi Mwananchi wa kawaida niogope kwenda ndani kama sababu ya msingi ni kukataa uonevu au dhuluma...

Comrade Lema... Kukaa kwako ndani kumewatoa watu wengi hofu ya kutokukata tamaa ya kupigania mageuzi kwakuwa huko nako wanaishi binadamu wala siyo wanyama...

Comrade Lema.... Nakutakia ijumaa njema tutakutana jumanne Mahakamani nikiwa na makamanda wengi kutoka kila pembezoni ..... Ur Comrade Henry Kilewo
NEVER SAY NEVER

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright JAMIIYETU | Designed By BAKI NASI
Back To Top