Loading...
http://go.ad2up.com/afu.php?id=778977

BREAKING NEWS: SIRI NZITO YAFICHUKA PROF LIPUMBA AUMBUKA VIBAYA ABAINIKA KUHUSIKA TUKIO HILI ZITO LA KIKATILI.

Sasa si siri tena,kuwa wale waliovamia mkutano wa CUF-Maalim pale Vinna Hotel Mabibo,ni wafuasi wa Profesa Lipumba na zoezi zima liliongozwa na Kambaya toka ofisi za chama Buguruni.

Walioshiriki zoezi hilo,wengi ni wale waliohusika "kuuvuruga" mkutano wa CUF pale Ubungo Plaza wakati Prof Haruna Lipumba alipoamua kuingia kwa nguvu,kuvuruga mkutano,kuvunja viti na kuzabua watu makofi.

Aliyevunjwa mguu kwa kudhaniwa ni "jambazi" na wale "wananchi wenye hasira kali" ni mlinzi wa Prof Lipumba ambaye amekuwa naye katika mikutano na misafara mingi azungukayo Dsm na nje ya Dsm.Hata alipopigwa na kupigika,aliomba msamaha kwa kusema yeye aliyumwa tu na Prof Lipumba,anaomba raia wasimuuwe.

Gari mbili aina ya Land Cruiser zilizotumika kuvamia eneo la Hotel na kutokomea mara baada ya wananchi kuingilia kati,zimekutwa ofisi za CUF-Buguruni ambazo kwa sasa zipo chini ya himaya ya CUF ya Lipumba na wafuasi wake chini ya Abdul Kambaya.Magari yote yamevunjwa vioo na kujaa damu zilizotokana na vipigo toka kwa wananchi.
Msemaji wa CUF ya Lipumba ndugu Kambaya yeye alipoulizwa,kwanza alikubali kuwa magari hayo ndiyo yalikuwa Vina Hotel-Mabibo,na walioanza kuyavamia ni wafauasi wa Chadema waliokodishwa toka Arusha kuja kuivuruga CUF ya Lipumba,anasema ni kweli magari hayo na watu waliokuwa ndani yake walivamiwa na wahuni wa CHADEMA walioletwa toka Arusha kwa ufadhiri wa Meya wa Ubungo kuja kumuondoa Lipumba ofisini.

Kambaya anasema vijana wa CHADEMA waliotolewa Arusha kuja kuleta vurugu Buguruni,ndio walianza kuwavamia walinzi wa CUF waliokuwa katika doria ya kawaida ya kuangalia wapi CHADEMA na vijana wao wanakutana ili kutengeneza fitna za kumuondoa Prof Lipumba kwa nguvu pale Buguruni.

Kambaya anasema wao kama CUF hawatakubali uhuni huo uliofanywa na CHADEMA na Meya wa Ubungo kwa kushirikiana na Maalif Seif,wao kama vijana wapo tayari kukilinda chama chao kwa nguvu zote,wapo tayari kulipa kisasi na kusimamia chama chao.

Abdul Kambaya anasema magari hayo ya chama yapo ofisi za CUF Buguruni na wanayaacha kama ushahidi wa namna wahuni wa CHADEMA toka Arusha wakishirikiana na Meya wa Ubungo wanavyotaka kuivuruga CUF kwa pesa za mafisadi.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright JAMIIYETU | Designed By BAKI NASI
Back To Top