Loading...
http://go.ad2up.com/afu.php?id=778977

HATARI SANA EDO KUMWEMBE AWATUSI YANGA KIANA AFUNGUKA MAZITO JUU YA YANGA KUPITISHA BAKULI.

Jumatatu ya April 24 klabu ya Yanga ilizindua mpango wa kuomba mashabiki na wanachama kuichangia timu yao ili kuiwezesha kiuchumi, kila mmoja anafikiria wazo lake lakini moja kati ya watu ambao wamelipokea kwa utofauti ni mchambuzi mahiri wa habari za michezo wa Gazeti la MwanaSpoti Edo Kumwembe.
Haya ni mawazo ya Edo Kumwembe kupitia ukurasa wake wa facebook kuhusiana na suala la Yanga kuomba ichangiwe kwa njia ya simu na mashabiki wake.
“Yanga inaomba mchango kwa mashabiki wake? What a shame…mchango wa mashabiki wa Yanga ni kununua jezi original za timu na bidhaa kedekede zinazoambatana na jina lao. Mmewapelekea? Hapana. Mchango wa mashabiki wa Yanga ni kwenda kwa wingi viwanjani timu yao inapocheza ili wadhamini wajue ukubwa wa Yanga waipapatikie”
“Ni kweli mashabiki wanajitokeza na wadhamini wanaitamani Yanga, mdosi anabana ili aabudiwe, kamuulizeni jinsi Tiboroha alivyotimuliwa na mipango yake…kwa kuipenda Yanga tu kwa wingi wao tayari ni mchango tosha…walihitaji viongozi wa kutumia fursa hiyo Yanga iwe matawi ya juu sana”
“Leo viongozi wamerudi kwa mashabiki kutaka buku, nini maana ya kiongozi kama anashindwa kufikiria kuifanya Yanga iwe Tajiri? Yanga ya leo inaweza kuanzisha tournament ya siku tano tu ya pre season kwa kuziita Gor Mahia, Azam na Mamelodi ikauza TV rights kwa pesa kibao, ikapata wadhamini wa Tournament, ikapata viingilio vyote”

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright JAMIIYETU | Designed By BAKI NASI
Back To Top