Loading...
http://go.ad2up.com/afu.php?id=778977

HII NI KALI YA MWAKA KIKOSI KAZI CHA MH MAJALIWA CHAMLIZA LEMMA BUNGENI AFUNGUKA MAZITO MNO.




Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameibariki Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuendelea kuwatumia TAKUKURU pamoja na Jeshi la Polisi wenye silaha za moto wakati wanapokwenda kukusanya mapato pamoja na kodi kwa wafanyabiashara ambao ni wanadaiwa sugu.

Akijibu swali la Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini Godbless Lema katika kipindi cha maswali kwa Waziri Mkuu Bungeni Mjini Dodoma, amesema ni sahihi kwa kikosi kazi hicho (task force) kutumika kwa kuwa wapo baadhi ya wafanyabiashara sugu wenye lengo baya la kutotaka kulipa madeni na badala yake hutoa rushwa.

Mhe. Lema alitaka kusikia kauli ya serikali juu ya mfumo unaotumiwa TRA wa kusumbua na kuwatisha wafanyabiashara katika shughuli zao za kila siku huku ikiwa inadaiwa kuwa mamlaka hiyo hutumia Jeshi la Polisi, Usalama wa Taifa na TAKUKURU katika miji mikubwa ikiwemo Dar es Salaam, Mwanza , Arusha na Mbeya.

“Ni kweli kwamba tunacho chombo ambacho kinachowajibika katika ukusanyaji wa mapato na kodi kutoka kwa walipa kodi wetu wafanyabiashara wakiwemo, lakini TRA kutumia ‘task force’ haina maana ya kuwatishia amani wafanyabiashara ila lengo lake ni kufuatilia wadaiwa sugu japokuwa siyo wote ila wachache hawataki kabisa kulipa pamoja na kwamba wanajua wao ni wadaiwa sugu..... Tunatumia TAKUKURU kwa sababu kuna wengine hutumia fursa hiyo kutaka kuwahonga maafisa wa TRA ili wafutiwe madeni yao”. Alisema Majaliwa

Vile vile Majaliwa amesema ‘task force’ imeundwa na TRA wenyewe ili kuona wanapokwenda kukusanya madeni yao hakutumiki vitendo ambavyo havikubariki kama vile utoaji wa rushwa ili madeni hayo yasilipwe au namna nyingine yoyote ambayo mfanyabiashara anaweza kuona si sahihi kwake

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright JAMIIYETU | Designed By BAKI NASI
Back To Top