Loading...
http://go.ad2up.com/afu.php?id=778977

FAHAMA NJIA HIZI ZAKULINOGESHA PENZI LAKO KWAKE DAIMA...


KUPITIA safu hii uipendayo, leo ninakupa njia nne zitakazolifanya penzi lako liendelee kunoga, hata kama litakuwa limeanza kufubaa utaliamsha upya.

Wengi wamekuwa hawaelewi mambo mengi kuhusu uhusiano ndiyo maana huishia kulalamika kwamba wanapenda sana lakini mwisho wa siku huishia kutendwa.

Hakuna mtu ambaye hahitaji faraja, kila aliyekuwa na mpenzi wake anahitaji kuwa na furaha. Hakuna mtu ambaye anaingia kwenye mapenzi ili apate msongo wa mawazo, kila mtu anayediriki kuutoa moyo wake, kitu cha kwanza anachokitarajia ni faraja kisha furaha.

Ipo hivyo! Watu wengi wanakuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi huku wakiwa na matumaini kwamba hao waliokuwanao inawezekana watakuwa wapenzi wa maisha yao yote. Pasipo kujua, wakati mwingine kuna makosa hufanyika, mtu hajui afanye nini ili penzi alilonalo kwa mpenzi wake linoge, hajui ni njia zipi zitamfanya kupendwa kila siku.

Leo nitakutajia njia chache ambazo kama utazifanya, nakuhakikishia penzi lenu litashamiri zaidi ya lilivyo hivi sasa.

MPE UHURU KWANZA

Kila mtu anapenda kuwa huru, kuachwa afanye mambo yake anayoyapenda. Hakuna mtu anayependa kuingiliwa, hasa kwenye masuala ya kutumia simu yake. Kama kweli unahitaji penzi linoge, usitake kuingilia mambo yake hasa katika matumizi ya simu, unachotakiwa ni kumwambia muda ambao hupendi kuona akizungumza na simu na si kwamba kila unapoona simu yake inaita, unaichukua kwa nguvu.

Mapenzi hayapo hivyo, mpe uhuru mwenza wako. Haimaanishi mtu kama hajatulia basi kuchukua simu muda wote inapoita ndiyo kutamfanya kutulia, hapana, bali kwa kufanya hivyo utampa mbinu nyingine ya kuweza kupambana nawe. Unachotakiwa ni kumfanya kuwa huru, usimuingilie.

CHUKUA MUDA WAKO KUMTOA ‘OUT’

Wengi hukosea hapa, huwa hawapendi kwenda matembezi na wapenzi wao. Wengine hujifanya wapo bize, hata ukimwambia Jumamosi nataka tutoke out atakwambia anataka kufanya hili na lile.

Rafiki yangu, kila mtu anahitaji kuwa karibu na mpenzi wake, hakuna anayependa kuwa na mpenzi ambaye muda wote yupo bize tu. Mchukue, nenda naye sehemu. Kutoka mitoko ya mara kwa mara itawafanya muwe karibu zaidi, itawafanya muda wote mzidi kupendana, ila kama utajifanya upo bize, jua kuna mtu ataitumia nafasi hiyo kutoka na umpendaye.

PENDELEA KUFANYA UTANI

Hakuna mtu anayempenda mpenzi ambaye yupo siriazi saa ishirini na nne. Pata muda wa kukaa na kutaniana naye. Mchombeze kwa vineno vya utani, mpetipeti, mlaze kitandani na uanze kupiganapigana naye vibao vya kimahaba hata kwa kutumia mito ya kulalia.

Unapokuwa siriazi kila wakati inakuwa ni vigumu mwenzako kulifaidi penzi, pendelea kutabasamu inapobidi kila unapokuwa na mpenzi wako, siyo kila atakachokwambia wewe uso wako umekunja ndita kiasi kwamba ataonekana kukuogopa na kumtafuta mtu mwingine ambaye atahitaji kuliona tabasamu lake, atahitaji kuona akifanyiwa utani wa mahaba nk.

HEBU MSIFIESIFIE BASI

Wengi wanaogopa kuwasifia wapenzi wao, hawajui kama kila mtu duniani anapenda kusifiwa. Mpenzi wako anapovaa nguo nzuri zilizomtoa, usikae kimya, mwambie amependeza kwani hilo litamfanya kufurahi sana. Kama utakuwa na mpenzi halafu kila siku humsifii hata akifanya kitu gani, jua kwamba atajisikia vibaya, wakati mwingine atahisi hayupo sawa kwa kuwa tu hujawahi kumsifia.
Unapomsifia mpenzi wako kunamfanya kuongeza umakini katika kuvaa kwake, kununua manukato na hata jinsi atakavyosuka au kunyoa atafanya kwa ubora wa hali ya juu kwa kuwa anajua utamsifia

BREAKING NEWS: MAAMUZI MAZITO YA KISHERIA YAMUWEKA PABAYA KIKWETE HAKUNA ALIEAMNI HILI..


Nimeona kwenye mitandao ya kijamii  baadhi ya wachangiaji wakimdhihaki Tundu Lissu kwamba anachemka kusema Kikwete ahojiwe. Wapingaji hawa wanashangaa uanasheria wa Tundu Lissu kwamba iweje hajui kama Kikwete ana kinga. Tundu Lissu. Wabongo wavivu kusoma, naomba niweke Ibara ya 46 na Ibara ndogo zake tujadili namna ya kumdaka Jakaya Kikwete


46.-(1) During the President’s tenure of office in accordance with this
Constitution it shall be prohibited to institute or continue in court any criminal proceedings whatsoever against him.

(2) During the President’s tenure of office in accordance this Constitution, no civil proceedings against him shall be instituted in court in respect of anything done or not done, or purporting to have been done or not done, by him in his personal capacity as an ordinary citizen whether before or after he assumed the office of President, unless at least thirty days before the proceedings are instituted in court, notice of claim in writing has been delivered to him or sent to him pursuant to the procedure prescribed by an Act of Parliament, stating the nature of such proceedings, the cause of action, the name, residential address of the claimant and the relief which he claims.

(3) Except where he ceases to hold the office of President pursuant to the provisions of Article 46A(10) it shall be prohibited to institute in court criminal or civil proceedings whatsoever against a person who was holding the office of President after he ceases to hold such office for anything he did in his capacity as President while he held the office of President in accordance with this Constitution.

UFAFANUZI
Ibara hii inazungumzia Kinga anayopewa Rais. Ibara ya 46 ibara ndogo ya 3, inasisitiza hatashitakiwa kwa makosa aliyofanya katika kipindi akiwa Rais na si vinginevyo. Hivyo Kikwete anaweza kudakwa kwenye makosa aliyofanya akiwa Waziri wa Nishati na Madini.

NYONGEZA
Kwa hiyo hata kwa katiba hii,hata Rais Magufuli akitolewa madarakani 2020 tunaweza kumuundia kamati na kumshitaki kwa makosa ya MV Dar es Salaam na uuzwaji wa nyumba za serikali.

MY TAKE
Nadhani Magufuli hakujua kama wale ''wahuni'' kina Tundu Lissu watamfikisha huku, matokeo yake anaweza kurudi nyuma ikawa kama zile kamati zingine zilizopita

HABARI NZITO: NI HATARI WEMA SEPETU KUANDIKA HISHORIA NZITO MAHAKANI HII LEO...


Kesi ya kukutwa na dawa za kulevya inayomkabili Wema Sepetu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeahirishwa hadi Julai 10.

Wema ambaye ni mshindi wa taji la urembo, maarufu Miss Tanzania kwa mwaka 2006 na msanii wa filamu, anakabiliwa na kesi hiyo akidaiwa kutumia na kupatikana na bangi.

Wakili wa Serikali, Elizabeth Mkunde mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa alisema kesi ilipangwa leo (Jumatano) kuanza kusikiliza ushahidi wa upande wa mashtaka lakini Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba anayeisikiliza kesi hiyo yupo likizo.

Kutokana na hilo, aliomba iahirishwe hadi Julai 10 ombi lililokubaliwa na mahakama.

Wema na wenzake Angelina Msigwa na Matrida Abbas wanakabiliwa na mashtaka mawili ya kukutwa na dawa za kulevya na kutumia dawa hizo.

Inadaiwa Februari 4, katika makazi ya Wema, Kunduchi Ununio, walikamatwa wakiwa na msokoto mmoja na vipisi vya bangi vyenye uzito wa gramu 1.08.

Wema pia anadaiwa Februari Mosi katika eneo lisilojulikana jijini Dar es Salaam alitumia bangi.

HOT NEWS: KIMENUKA BUNGENI SPIKA NDUGAI, KAMBI YA UPINZANI WAKABANA MAKOO SHUHUDIA TUKIO HILI HAPA..

Bungeni
Spika wa Bunge, Job Ndugai amewakumbusha wabunge wa upinzani wanaotaka marais wastaafu washtakiwe kuhusu sakata la mchanga wa madini, wakumbuke wanao mawaziri wakuu wastaafu wawili ambao watahusika pia.

Ndugai amesema hayo leo (Jumanne) bungeni baada ya mchango wa Mbunge wa Kilombero, Peter Lijualikali kusema haiwezekani mawaziri na watendaji wengine wa Serikali wakafanikisha mikataba mibovu ya madini bila ridhaa ya Rais.

"Haiwezekani mzee wangu (Andrew) Chenge na (Nazir) Karamagi walipitisha mikataba hiyo bila Rais aliyekuwapo kufahamu. Kinga ya Rais kushtakiwa iondolewe ili wahojiwe," amesema Lijualikali.

Baada ya hoja hiyo ya Lijualikali inayofanana na ya Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Ndugai aliwakumbusha juu ya mawaziri wastaafu walionao kwenye chama chao.

"Mabadiliko mnayoyataka yakipitishwa na viongozi mlionao wakikamatwa msije mkalalamika tena," amesemaNdugai.

HABARI NZITO: JUMA KASEJA ATOBO SIRI NZITO YA MANULA BOCCO NA KAPOMBE KUIHAMA AZAMA FC...

Golikipa wa zamani wa timu za Simba na Yanga ambaye kwa sasa anaichezea Kagera Sugar ya Bukoba Juma Kaseja alikuwa ni mmoja kati ya wageni waliyoalikwa katika kipindi cha Sports Bar cha Clouds TV kuzungumzia masuala mbalimbali kuhusiana na soka la Tanzania.
Juma Kaseja kama moja ya wachezaji wenye uzoefu ambao wamewahi kucheza vilabu vya Simba na Yanga kwa mafanikio makubwa, aliulizwa swali kuhusiana na mtazamo wake kuhusu Shomari Kapombe, Aishi Manula na John Bocco kutoka Azam FC kwenda Simba anafikiri ni wakati sahihi?
“Sijui kuna vitu gani vimetokea ndani ya Azam na mimi nasikia tu kama mnavyosikia nyie kuna utaratibu umewekwa hakutakiwa kusajili mchezaji sijui zaidi ya Milioni 15 lakini tunasikia Mbaraka kachukua zaidi ya Milioni 15”>>> Kaseja
Juma Kaseja

“Mimi nadhani tu kuna vitu vimetokea kwenye mpira wa Tanzania vinataka kuwaondoa wale wachezaji ambao wanaonekana ni waandamizi kwenye timu na hivyo vitu mimi sidhani kama viko Azam tu hivyo vitu vipo kwenye mpira wa Tanzania kwa hiyo Azam wamevitoa kwenye hizi timu kubwa mbili nao wamevipeleka kwao”>>> Kaseja
“Kwanza heshima watu hawataki kuwapa heshima wachezaji, Bocco ni mchezaji mkubwa ndani ya Azam anatakiwa wampe heshima yake hata kama kulikuwa kuna tatizo la mambo ya hela sijui kiuchumi wangeweza kukaa nae chini na kuongea nae Bocco nae ni binadamu” >>> Kaseja
“Kama miaka yote kachukua hela nyingi anawezaje kukataa mwaka mmoja, bwana sasa hivi uchumi umeyumba lakini mwakani mambo yakikaa vizuri haina neno Bocco nae ni binadamu angeelewa”>>>Kaseja
“Unapokuja kumfanyia mchezaji mkubwa kama huyo ambaye kashajitolea sana kuisaidia timu kibinadamu hata yeye hawezi kuwa na furaha anaona kadharaurika na hivyo ni vitu ambavyo wamefanyiwa watu wengi sema kwa Azam Bocco ndio mchezaji wa kwanza lakini kwa hizi timu zingine kawaida” >>> Kaseja

ZITO KABWE AKINUKISHA TENA ATUMA UJUMBE MZITO KWA RAIS MAGUFULI HAKUNA ALIEAMINI HAYA...


"Mwisho wa siku historia inaandikwa tu. Uzalendo ni kufanya jambo ambalo wengi hawakuelewi lakini wewe unajua Ni jambo sahihi na unakubali kutukanwa, kususubikwa, kusimangwa, kuzushiwa, nk. Unapambana tu. Mwisho wa siku waliokuita msaliti watakuita shujaa. Waliokuzomea wanashangilia. Wewe unafanya nini? Unakaa kimya kwani kwenye kukaa kimya pia kuna kusema kukubwa zaidi. Muhimu Nchi ifaidike.

Huko nyuma nilipata kusema, hata mungu akinichukua sasa unakwenda ukiwa umetabasamu kwani unakuwa umetimiza wajibu wako duniani. Kina Josina Umm Kulthum wataishi Kwa heshima inshallah"

Ameandika Zitto Kabwe kupitia ukurasa wake wa Facebook mara baada ya ripoti ya pili ya mchanga wa madini kuwasilishwa

BREAKING NEWS: KIMENUKA RIPOTI YA PILI MCHANGA WA MADINI CHENGE ,NGELEJA NDIO BASI TENA YAWAKUTA MAZITO..


Ripoti ya kamati ya pili kuhusu mchanga wa madini imewaibua Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge na Mbunge wa Sengerema, Wiliam Ngeleja kuhusu mikataba ya madini iliyoingiwa miaka iliyopita.

Mbali na hao pia imewaibua marehemu Dk Abdallah Kigoda aliyekuwa Mbunge wa Handeni na Daniel Yona aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini.

Majina ya viongozi hao yameibuka leo wakati  mwenyekiti wa kamati hiyo, Profesa Nehemiah Osoro alipokuwa akiwasilisha matokeo ya ripoti yake.

DONE DEAL: AISHI MANULA AIHAMA AZAMA FC LEO ATIMKIA UPINZANI YANGA WAFUNGUKA MAZITO...





Baada ya tetesi za muda mrefu kuhusiana na golikipa wa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars anayeichezea club ya Azam FC Aishi Manula kuhusishwa kuwa muda wowote anaweza ihama club hiyo na kwenda kujiunga na Simba huku Singida United ikitajwa kumuwania pia.

Leo June 11 2017 taarifa kutoka katika mtandao wa habari za michezo Tanzania Shaffihdauda.co.tz umetangaza kuwa golikipa Aishi Manula amejiunga na club ya Simba kwa mkataba wa miaka miwili kwa ada ya usajili ya Tsh milioni 50.

HABARI NZITO: PAUL MAKONDA KWELI KIBOKA AMWAGA MABILIONI KATIKA JAMBO HILI ZITO MNO..



Ikiwa ni nje ya Zawadi zilizokuwa zimeandaliwa kwajili ya Washindi wa mashindano makubwa afrika ya kuhifadhi na kusoma Qur-an juzuu 30 Kati ya washiriki 17 kutoka nchi 15 Barani Afrika yaliyofanyika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es salaam, Tanzania, Katika hotuba yake Mkuu wa mkoa wa jiji hilo Paul Makonda naye kwa upande wake alitamka kuongeza shilingi Milioni 5 kwenye zawadi za washindi watano waliopatikana.

Mohamed Abdullah Aden kutoka Somalia ndiye ameibuka mshindi wa mashindano makubwa Afrika ya kusoma na kuhifadhi Qur-an juzuu 30 amekabidhiwa hundi ya Shilingi Milioni 15 kutoka Amana Bank, halikadhalika amepewa cheti cha ushindi, Ipod na kuchagua kwenda nchi yeyote duniani, kijana huyo wa miaka 12 ametoa wito kwa vijana kujibidisha Katika kusoma Qur-an.

Mashindano hayo ya 18 yaliyo andaliwa na Taasisi ya Al-hikma Foundation yamehudhuriwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kasim Majaliwa, Mufti Mkuu wa Tanzania Abubakar Zubeiry, Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda, Skeikh Mkuu Dar es salaam Alhad Mussa Salum, Rais mstaafu Ali Hassani Mwinyi Sambamba na ujumbe Maalumu kutoka nchini Saudiarabia.

BREAKING NEWS: HABARI ZILIZOTUFIKIA HIVI PUNDE RAIS MAGUFULI NDIO BASI TENA AIBUA SAKATA ZITO MNO NCHINI...




Siku chache tangu akabidhiwe ripoti ya mchanga wa madini, Rais Magufuli atapokea taarifa ya kamati ya pili ya wachumi na wanasheria iliyofanya uchunguzi madini yaliyo kwenye makontena yenye mchanga wa madini Jumatatu June 12, 2017 Ikulu Dar es Salaam.

AyoTV na millardayo.com zitakuletea tukio hili moja kwa moja  kwenye Youtube ya millardayo kuanzia saa 3:30 Asubuhi.

Older Posts
© Copyright JAMIIYETU | Designed By BAKI NASI
Back To Top