Hisia kama tulivyoona ni tabia ya kimaumbile aliyonayo mtu. Kila mtu ana tamaa ya kupata mafanikio katika maisha yake. Hiyo ni hisia haina hoja ya msingi katika kuleta mafanikio. Mafanikio ili yapatikane lazima iwepo hoja ya msingi itakayo tawala katika maneno na vitendo vya mtu katika maisha ya mtu. Kivipi kuwe na hoja za msingi?
Ukitaka mafanikio lazima ujenge hoja za msingi na zenye mashiko. Ni lazima uwe tayari kuizishinda hisia za matamanio katika maisha. Uamue kuifanya akili yako iongozwe na hoja badala ya kuongozwa na hisia.
Hoja humfanya mtu kuwa na uhakika wa kile anachokifanya. Kuwa na ‘data’ sahihi za kile anachofanya. Humfanya mtu kufanya kila kitu kwa ufanisi MKUBWA.
Hoja humfanya mtu kujiamini na kuthamini kile anachofanya. Hoja humpa heshima na kumfanya athaminike na jamii kutokana na kufanya vitu sahihi na vyenye tija kwa jamii.
Hisia au tamaa humfanya mtu kufanya maamuzi yanayompelekea kujuta baadae katika maisha take.
Hisia zikimtawala mtu hufanya vitu vya aibu na kumdhalilisha katika jamii kama kuiba, kubaka, kulawiti, kusema uongo kwa manufaa binafsi, kula mali ya haramu bila Hofu. Hisia zikimtawala mtu hukosa kujiamini na kujiona mwenye mapungufu na kukosa ujasiri.
Katika kumalizia somo letu naomba kutoa angalizo kuwa kabla ya kufanya maamuzi katika jambo lolote unalohitaji kufanya kwanza jiulize unayotaka kufanya je, yanaongozwa na hisia au hoja? Kama yanaongozwa na hisia au tamaa kamwe usifanye jambo hilo na kama jambo hilo linaongozwa na hoja hakika lifanye maana litakufaa katika maisha yako.
Post a Comment