Loading...
http://go.ad2up.com/afu.php?id=778977

HABARI NZITO: PAUL MAKONDA KUTAJA LISTI NYINGINE VINARA MADAWA YA KULEVYA.


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda leo anatarajia kutaja majina mengine ya vinara wanaotuhumiwa kwenye biashara ya madawa ya kulevya.



Katika awamu ya pili, watu mashuhuri wakiwemo Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, Askofu Josephat Gwajima na mbunge wa zamani wa Kinondoni, Idd Azzan walitajwa.

“Awamu ya tatu imekamilika naomba tukutane kesho katika ukumbi wa mwalimu nyerere kuanzia saa 4 asbh,” mkuu huyo wa mkoa aliandika jana kwenye Instagram.

Jana Rais Dkt John Magufuli aliwataka viongozi kuongeza nguvu kwenye mapambano ya biashara hiyo haramu

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright JAMIIYETU | Designed By BAKI NASI
Back To Top