Loading...
http://go.ad2up.com/afu.php?id=778977

UKWELI MCHUNGU RAIS MAGUFULI AMEENDA KINYUME NA MITAZAMO YA WANANCHI.

Bila shaka mmepatwa na mshangao kwa uamuzi uliochukuliwa dhidi ya msanii Ney wa Mitego. Nimejaribu kupitia matukio kadhaa yaliyotokea hivi karibuni ndani ya nchi yetu Tanzania yaliyokua yanategemea maamuzi kutoka kwa mh rais. 

Nimegundua rais amekua akitenda tofauti na mitazamo/hukumu zetu. Mfano tukianza na swala la Mkuu wa Mkoa wa Dar na tuhuma dhidi ya kugushi vyeti na kuvamia Clouds matumaini na mitizamo yetu ilikua ni kwamba mh rais angemuondoa ktk nafasi yake na kuchukuliwa hatua za kisheria lakini kachukua maamuzi ambayo kila mtu hadi sasa amebaki na mshangao. 

Ukija katika ishu ya Ney wa Mitego kuhusu wimbo wake kuoneka kuwa na baadhi ya maneno yanayomlenga mh rais watu wengi walishatoa hukumu kuwa msanii huyu. atafungwa au kupotezwa kabisa hasa baada ya msanii huyo kukamatwa na Jeshi la Polisi mjini Morogoro lakini imekua tofauti pia na uamuzi aliochukua mh rais wa kuagiza msanii huyo aachiwe na wimbo wake uendelee kupigwa na vituo vyote vya redio nchini hivyo kutengua uamuzi wa BASATA walioufungia wimbo huo.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright JAMIIYETU | Designed By BAKI NASI
Back To Top