Loading...
http://go.ad2up.com/afu.php?id=778977

MOURINHO AMPA MAKAVU RONALDO NA KUSEMA...HAZARD NI BORA KULIKO RONALDO-MOURINHO



Meneja wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amempiga dongo mshambuliaji kutoka nchini Ureno pamoja na klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo kwa kumtofautisha na kiungo mshambuliaji kutoka nchini Ubelgiji, Eden Hazard.

Mourinho ambaye yupo njiani kurejea nchini England sanjari na kikosi chake akitokea nchini Marekani walipokua wameweka kambi ya kujiandaa na msimu mpya wa ligi, amesema Hazard ni mchezaji bora zaidi kuliko Ronaldo kutokana na uchunguzi wake alioufanya.

Meneja huyo kutoka nchini Ureno amesisitiza kuwa na uhakika wa jambo hilo ambalo alilizungumza mbele ya waandishi wa habari huko nchini Marekani huku akimuweka Ronaldo katika nafasi ya tatu kwa ubora duniani.

Alisema kwa soka la sasa ni vigumu kumfananisha Ronaldo na Hazard, hasa ikizingatiwa kiungo huyo wa klabu ya Chelsea msimu uliopita alikua lulu kwenye kikosi chake hadi kufikia hatua ya kutajwa kama mchezaji bora wa mwaka huko nchini England.

Mourinho, alikamilisha kwa kubainisha kwamba endapo akipewa nafasi ya kutaja walio bora duniani kwa sasa mchezaji wa kwanza kwake atakua Lionel Messi, kisha Eden Hazard halafu Ronaldo atafuatia.

Hata hivyo imekua ikiripotiwa kwamba Mourinho amekua hana mahusiano mazuri na Ronaldo wanapokua nje ya uwanja licha ya kuwahi kufanya kazi kwa pamoja huko mjini Madrid wakati meneja huyo alipokua mkuu wa benchi la ufundi la Real madrid.

Kabla ya Mourinho kwenda kukinoa kikosi cha Real Madrid, mara kadhaa aliwahi kumchokonoa Ronaldo kupitia vyombo vya habari lakini mshambuliaji huyo hakumjibu chochote zaidi ya kuendelea na shughuli zake za kucheza soka.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright JAMIIYETU | Designed By BAKI NASI
Back To Top