Loading...
http://go.ad2up.com/afu.php?id=778977

BREAKING NEWS: HII NI LAANA YA KUTISHA BUNGE LAWEZA KUIBUA KASHFA CHAFU NCHINI ZIDI KIONGOZI HUYU...

Image result for ANDREW CHENGE

BUNGE limenusa ufisadi katika Ofisi ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali baada ya kubaini kuna mashine ya uchapaji ilinunuliwa kwa gharama kubwa, ikafanya kazi kwa muda mfupi na mpaka sasa, haifanyi kazi.

Aidha, Bunge limebaini ofisi hiyo haina usiri wa nyaraka za serikali zinazochapwa kwa kuwa baadhi ya nyaraka zinachapwa nje ya ofisi na inajiendesha chini ya viwango.

Waliishauri Serikali ifanye mabadiliko ya Menejimenti kwa kuwa muda mrefu hakuna ufanisi, taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo ilieleza hayo.

Taarifa hiyo iliridhiwa na Bunge bila kujadiliwa na wabunge juzi wakati Mwenyekiti wake, Andrew Chenge alipokuwa akifanya majumuisho mafupi bungeni mjini hapa.

Taarifa hiyo iliwasilishwa Alhamisi, Novemba 10 na Makamu Mwenyekiti wa kamati na Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja (CCM) lilipaswa kujadiliwa juzi lakini haikuwezekana kutokana na kifo cha Mbunge wa Dimani, Hafidh Ali Tahir (CCM) kilichotokea ghafla usiku wa kuamkia juzi mjini hapa.

Pia shughuli za Bunge ziliahirishwa mara mbili katika Mkutano huo wa Tano wa Bunge la 11, kutokana na kifo cha Spika Mstaafu wa Bunge la Tisa, Samuel Sitta.

Akiwasilisha taarifa hiyo ambayo ilifanyiwa majumuisho mafupi na Chenge juzi, Ngeleja alisema Kamati hiyo ilifanya ziara katika Ofisi ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali Machi 15 mwaka huu na kujionea shughuli za ofisi hiyo za uchapaji wa nyaraka za serikali, zikiwemo Sheria Ndogo.

“Hata hivyo Kamati hii imebaini kuwa Idara hii haiendeshwi kwa viwango vinavyokidhi mahitaji yaliyopo. Kwa mfano katika vikao vya Kamati vilivyopita, Kamati haikupokea kwa wakati Sheria Ndogo mbalimbali kwa sababu hazikuwa zimechapwa na Mpiga Chapa wa Serikali,” alisema Ngeleja.

Kamati hiyo ilisema kuwa dosari hiyo inatokana na ukweli kwamba ofisi hiyo inatekeleza majukumu yake chini ya kiwango kinachotakiwa na iko nyuma kiteknolojia.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright JAMIIYETU | Designed By BAKI NASI
Back To Top