Loading...
http://go.ad2up.com/afu.php?id=778977

HABARI NZITO YA HIVI PUNDE: NI PIGO ZITO KWA RAIS MAGUFULI HAKUNA ALIETEGEMEA KUSIKIA KAULI HIZI NZITO


Rungwe, ambaye aligombea urais mwaka jana na kushika nafasi ya tano akiwa amepata asilimia 0.32 ya kura, alisema hayo alipofanya mahojiano na gazeti hili ofisini kwake jijini.
Rungwe alikuwa akizungumzia mwaka mmoja wa Magufuli, akisema kinachofanywa na Rais pamoja na wateule wake ni kutaka kuonyesha wanafanya vizuri kuliko watangulizi wao.
“Nasikia kelele na ukosoaji wa kila kilichofanywa kabla ya utawala huu. Ni hulka ya binadamu kudhani kuwa kila wazo lake ni bora kuliko wengine na atapenda kulitekeleza, hata ikimaanisha kwenda kinyume na taratibu zilizopo,” alisema Rungwe.
Pamoja na mtazamo huo, Rungwe alikiri kuwapo kwa maendeleo yaliyotokana na juhudi binafsi kwa kila mwananchi, huku akikosoa mambo mengi yanayofanywa na ama Rais mwenyewe au wasaidizi wake.
Alikumbusha kauli aliyoitoa Rais wakati akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika kisiwani Unguja kushukuru wananchi kwa kumchagua kwenye Uchaguzi Mkuu uliopita kuhusu kitendo cha katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad kukataa kumpa mkono Rais wa Zanzibar, Dk Mohammed Shein kwenye mazishi ya aliyekua Rais wa Awamu ya Pili wa Zanzibar, Abood Jumbe.

Siku hiyo, Rais Magufuli alisema: “Mtu mmekutana kwenye msiba, mahali kwenye majonzi, mnamsindikiza marehemu. Kwa unyenyekevu wako Dk Shein ukatoa mkono wako kumsalimia mtu fulani. Huyu mtu akakatalia mikono yake na bado asubuhi yake ukasaini fomu zake za kwenda kutibiwa nje ya nchi.
“Haya ni mapenzi makubwa sana. Amekataa mkono wako. Huyohuyo akiugua unampeleka hospitali. Akitaka kusafiri nje, unasaini na unampa na fedha na posho za kwenda nje. Mimi nisingeweza.”
Pia Rungwe alikumbusha pia tukio lililojiri wakati wa uzinduzi wa Daraja la Nyerere ambako Rais aliwauliza wananchi kama amtumbue au asimtumbue aliyekuwa mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, marehemu Wilson Kabwe.
“Hizi ni tabia binafsi. Hatuhitaji kuzifahamu. Tunataka uongozi kwa kutumia sheria tulizonazo. Rais hafahamu tofauti hiyo. Urais ni tofauti na tabia zake ambazo anaweza akazifanya akiwa na familia yake au watu wake wa karibu,” alisema wakili huyo wa Mahakama Kuu.
Alisema kauli ya Rais kwamba angekuwa yeye asingesaini kuidhinisha malipo ya safari ya matibabu ya Maalim Seif baada ya kukataliwa kutoa mkono wa salamu, haina maana kwa kuwa hasira humpata mtu yeyote na si vyema kuzionyesha mbele ya watu.
“Rais kuonyesha hasira kiasi hicho si vizuri. Maalim alikuwa kiongozi wa nchi hii na anayo haki kwa kila analostahili, si mpaka amfurahishe mtu fulani,” alisema Rungwe na kufafanua kuwa hali hiyo ya kutaka kufurahisha ndiyo inayosababisha kila mtu ajaribu kumfurahisha Rais hata kwa kuvunja haki za wengine.
Alisema ipo mifano hai ya viongozi waliokuwa na nia njema ya kuwasaidia wananchi wao, lakini wakashindwa kufanikisha malengo yao.
“Rais Magufuli anaelekea huko hivyo washauri wake wachukue hatua mapema kabla mambo hayajaharibika,” alisema Rungwe.
Mwenyekiti huyo wa chama ambacho hakijapata uwakilishi bungeni, alisema hata Rais wa Awamu ya Kwanza, Mwalimu Julius Nyerere alikuwa na nia njema ya kuijenga Tanzania ya ujamaa na kujitegemea hadi akaasisi Azimio la Arusha, lakini hakufanikisha ndoto yake.
Alitaja mfano mwingine kuwa ni Zimbabwe ambako uchumi unayumba kutokana na sera zinazotekelezwa na Rais Robert Mugabe. Alisema alipoikuta nchi hiyo ni tofauti na alipoifikisha.
“Nilienda Zimbabwe, hali ni tofauti sana. Uchumi umeharibika kutokana na msimamo wa Rais,” alisema.
Miongoni mwa masuala ya kiuchumi yaliyobadilisha uchumi wa taifa hilo, kwa mujibu wa Rungwe, ni kutaifisha mashamba makubwa ya walowezi na kuyagawa kwa wakulima wazawa jambo, lililolalamikiwa na wengi.
Kutokana na mifano hiyo, Rungwe alimtaka Rais Magufuli kukumbuka mahitaji ya wananchi wote badala ya kuelekeza nguvu nyingi kupambana na kundi dogo la wezi kwenye jamii.
Alisema licha ya uzuri wa kupambana na wizi, rushwa na matumizi mabaya ya viongozi, wananchi wengi wana njaa ambayo haiwezi kumalizika kama hakutakuwa na chakula mezani kwao.
“Wezi na wala rushwa wameandikwa hata kwenye vitabu vitakatifu. Lazima wawepo kwenye jamii yoyote, lakini huwezi kuwatafuta wezi 100 na kuathiri maisha ya zaidi ya Watanzania milioni 50,” alisema.
“Mishahara haijaongezeka, pensheni hazilipwi kwa wakati lakini wateule wote wa Rais wanaishi maisha mazuri. Wamebadilika tangu walipoteuliwa. Wengine walikuwa wanafunzi, lakini sasa wanaongea lugha tofauti. Wananchi wanahitaji chakula mezani si vita visivyokuwa na mwisho,” alisema.
Utumbuaji
Kuhusu utumbuaji, Rungwe alisema umekuwa ukifanywa kinyume na taratibu, jambo alilosema linaongeza chuki miongoni mwa watumishi na Serikali yao.
“Utumbuaji unatengeneza chuki baina ya watumishi wa umma na mwisho wa siku Rais awe tayari kuwaomba radhi watumishi anaowatumbua,” alisema.
Alielekeza lawama kwa washauri wa Rais kwamba hawatekelezi wajibu wao kama inavyotakiwa ndiyo maana anaweza kuongea vitu ambavyo haviendani na hadhi ya ofisi anayoihudumu.
“Rais ni kama baba wa familia. Hawezi kumdhalilisha mbele ya kadamnasi mwanaye aliyekosea. Wanachofanyiwa watumishi na wafanyabiashara si sahihi. Ndiyo maana hawajafikishwa mahakamani. Wapo watumishi wanaoendelea kulipwa mishahara na hawafanyi kazi,” alisema.
Katiba Mpya
Alisema Rais Magufuli hajaonyesha nia ya kukamilisha mchakato wa kuipata Katiba Mpya ambao ulianza wakati wa Serikali ya Awamu ya Nne na ukasitishwa kupisha Uchaguzi Mkuu.
“Rais hatakiwi kusitisha mchakato huo ambao ulianzishwa kwa baraka za chama chake na Watanzania wote wamekubali fedha zao zitumike kufanikisha hilo. Katiba na sheria ndizo zilizompa nafasi ya kuongoza nchi na si kitu kingine,” alisema.
Ila, alikosoa utaratibu uliotumiwa na Bunge Maaalum la Katiba (BMK) kupitisha Katiba inayopendekezwa kwa kupiga kura, akisema haikuwa sahihi.
“Tulijaa wanasiasa. Maamuzi yetu yalitokana na itikadi zetu. Katiba si suala la chama. Marekebisho yafanywe kuanzia pale,” alishauri.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright JAMIIYETU | Designed By BAKI NASI
Back To Top