Loading...
http://go.ad2up.com/afu.php?id=778977

Kubenea :Chadema Tunajivunia kwa Kuokoa Bilioni 1 za Kufua Majoho ..!!!

Mbunge wa Ubungo, Said Kubenea amesema tangu Chadema ichukue halmashauri mbalimbali jijini hapa imefanikiwa kuokoa Sh 1.2 bilioni zilizokuwa zinatumika kufua majoho ya madiwani Kinondoni na Ubungo kwa mwaka.

Kubenea ameyasema hayo leo wakati alipofanya mkutano wa hadhara uwanja wa Mabibo Farasi ikiwa ni ziara ya kwanza jimboni kwake tangu achaguliwe Oktoba 2015.

"Ubungo tumeokoa Sh 430 milioni zilizokuwa zinatumika kufua majoho 18 ya madiwani, Kinondoni Sh 800 milioni kwa majoho 58 na tangu Aprili mwaka jana hatujafua na hatujatoka upele," amesema Kubenea.

Kubenea amefanya ziara hiyo na itakuwa muendelezo wa kusikiliza kero za wananchi wa Jimbo la Ubungo.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright JAMIIYETU | Designed By BAKI NASI
Back To Top