Loading...
http://go.ad2up.com/afu.php?id=778977

HABARI NZITO: HII NI HATARI MBOE. MDEE NDIO BASI TENA WAKUTANA NA KIBANO KIZITO BUNGENI HIVI PUNDE.

MWENYEKITI wa Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe na mbunge wa Kawe Halima Mdee, jana wamehojiwa mbele ya Kamati ya Kudumu ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, inayoongozwa na Mbunge wa Newala Vijijini, George Mkuchika (CCM).

Mbowe ambaye pia ni wmenyekiti wa Chadema na Mbunge wa Kawe, Mdee walitakiwa kufika mbele ya Kamati hiyo kutokana na maagizo ya Spika wa Bunge, Job Ndugai aliyotoa bungeni Jumatano, Aprili 5, mwaka huu, akiwataka waripoti kwenye kamati hiyo siku iliyofuata.

Mbowe ambaye alikuwapo bungeni siku hiyo na Mdee ambaye hakuwapo, wote wawili wametii wito wa Spika, Ndugai wa kusimama mbele ya Mwenyekiti Mkuchika kuhojiwa kama ilivyokuwa imeagizwa na Spika wa Bunge wakitakiwakujibu tuhuma zinazowakabili. Mbowe inadaiwa alitoa lugha za matusi mtandaoni na Mdee anadaiwa kutoa lugha za matusi kwa Spika bungeni.

Mwenyekiti wa Chadema alifikishwa mbele ya Kamati hiyo akituhumiwa kufanya kosa la kulitukana Bunge mtandaoni baada ya wabunge wawili wa chama hicho kushindwa uchaguzi wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA).

Baada ya Ezekiel Wenje na Lawrance Macha waliokuwa wakiwania nafsi za ubunge wa EALA kupitia chama hicho kupata kura nyingi za hapana, Mbowe inadaiwa alianza kutukana bunge mitandaoni.

Habari za Mbowe kwamba alitukana mitandaoni ziliibuliwa na Mbunge wa Mwibara, Kange Lugola (CCM) ambaye aliomba mwongozo wa Spika kuhusu kiongozi huyo kutoa lugha za matusi mitandaoni akilitukana bunge sababu ya wabunge wake kukosa kura za kutosha kuchaguliwa kuingia EALA.

Spika Ndugai wakati akitoa mwongozo kuhusu jambo hilo, alimtaka Mwenyekiti Mbowe afike kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kujibu tuhuma hizo mara moja.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright JAMIIYETU | Designed By BAKI NASI
Back To Top