Loading...
http://go.ad2up.com/afu.php?id=778977

BREAKING NEWS: RAIS MAGUFULI KWELI TISHIO AINGIA KATIKA HISTORIA NZITO DUNIANI KAMA KIONGOZI WA KWANZA KUTOKA AFRIKA


KATIKA kipindi cha mwaka mmoja kilichoanzia Novemba mwaka jana mpaka Oktoba mwaka huu ambacho kimeongozwa na Serikali ya Awamu ya Tano chini Rais John Magufuli, jumla ya viwanda vipya 1,845 vimeanzishwa na hivyo kufanya jumla ya viwanda vyote nchini kufikia 54,422.

Hayo yalibainishwa hivi karibuni mjini Dodoma na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati akiahirisha Mkutano wa Tano wa Bunge la 11.

Waziri Mkuu Majaliwa alifafanua kuwa kwa mujibu wa ripoti iliyotokana na sensa ya viwanda iliyofanyika kuanzia mwaka 2013/14 hadi mwaka jana ilionekana kuwa mpaka Oktoba mwaka jana kulikuwa na viwanda 52,579.

“Ni matumaini ya Serikali kuwa kutokana na juhudi za uhamasishaji zinazofanyika, kasi ya uanzishwaji viwanda na hasa viwanda vidogo na vya kati na vikubwa itaongezeka sana,” alisisitiza Majaliwa katika hotuba hiyo ambayo hata hivyo hakuisoma bungeni kutokana na msiba wa Mbunge wa Dimani, Hafidh Ali Tahir, badala yake ikawekwa katika kumbukumbu rasmi za Bunge.

Alisema katika matokeo ya sensa hiyo hadi kufikia mwaka 2013, Tanzania ilikuwa na jumla ya viwanda 49,243 ambapo viwanda vidogo vinavyoajiri mtu mmoja hadi wanne vilikuwa ni asilimia 85.13 na viwanda vidogo vyenye watu watano hadi 49 vilikuwa asilimia 14.02.

Alisema matokeo hayo pia yalionesha kuwa viwanda vya kati vyenye watu 50 hadi 90 vilikuwa ni asilimia 0.35 na viwanda vikubwa vyenye watu kuanzia 100 na kuendelea ni asilimia 0.5.

Hivyo, Asilimia 99.15 ya viwanda vyote nchini ni viwanda vidogo.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright JAMIIYETU | Designed By BAKI NASI
Back To Top