Dar es Salaam. Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein leo saa nne asubuhi atasaini Muswada wa Sheria ya Uchimbaji Mafuta na Gesi Asilia wa mwaka 2016.
Taarifa kwa umma iliyotolewa jana na Dk Juma Mohammed Salum kwa niaba ya Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo (Zanzibar), Rais Shein atasaini muswada huo baada ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar kuupitisha kwenye Mkutano wa Tatu wa baraza hilo lililofanyika Septemba.
Imeelezwa kwenye taarifa hiyo kuwa, kusainiwa kwa sheria hiyo kutawezesha kazi ya utafutaji na uchimbaji wa mafuta na gesi asilia Zanzibar kuanza kwenye visiwa vya Unguja na Pemba.
Post a Comment