Loading...
http://go.ad2up.com/afu.php?id=778977

KUTOKA IKULU RAIS MAGUFULI RAIS AISHAMBULIA VIKALI TASNIA HII NYETI NCHINI NA KUANIKA UOZO WA KASHFA HII CHAFU NCHINI

RAIS John Magufuli amesikitishwa na uzushi unaofanywa kwa lengo la kumchafua Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete na familia yake, na amewataka waandishi wa habari na vyombo vya habari kuacha kuandika na kuchapisha taarifa za uzushi na badala yake vizingatie weledi na kufuata sheria.

Amesema taarifa zinazomhusisha kwamba amezuia mizigo ya mke wa Rais mstaafu Kikwete, Mama Salma Kikwete bandarini hadi hapo itakapolipiwa kodi, si kweli na ni uzushi, kwani hajawahi kuzuia wala kuagiza kuzuiwa kwa mizigo ya Mama Salma Kikwete.

Dk Magufuli aliyasema hayo katika taarifa iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, baada ya siku za karibuni, baadhi ya vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kuchapisha taarifa zinazomhusisha Mama Salma Kikwete na Taasisi anayoiongoza ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) kwamba imeshindwa kulipia kodi mizigo mikubwa iliyoiingiza nchini na hivyo kuwa hatarini kupigwa mnada.

Aidha, taarifa hizo zimemhusisha Rais Magufuli kuwa anahusika kuzuia mizigo hiyo bandarini mpaka hapo itakapolipiwa kodi.

“Tunapenda kuutaarifu umma kuwa taarifa hizo si kweli na ni uzushi, kwani Rais Magufuli hajawahi kuzuia wala kuagiza kuzuiwa kwa mizigo ya Mama Salma Kikwete,” ilieleza taarifa ya Ikulu.

“Rais Magufuli amesikitishwa sana na uzushi huo unaofanywa kwa lengo la kumchafua Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Dk Jakaya Kikwete na familia yake na amewataka waandishi wa habari na vyombo vya habari nchini kuacha kuandika na kuchapisha taarifa za uzushi na badala yake vizingatie weledi na kufuata sheria,” ilibainisha taarifa ya Ikulu na kuongeza:

“Nimesikitishwa sana na uzushi unaofanywa dhidi ya Rais mstaafu Jakaya Kikwete na mke wake Mama Salma Kikwete, tafadhali wale mnaotengeneza uzushi huu, acheni mara moja na muacheni Rais mstaafu Kikwete apumzike.

“Rais mstaafu Kikwete amefanya kazi kubwa ya kulitumikia Taifa hili, amestaafu anapumzika, narudia muacheni apumzike, Serikali haitaendelea kuvumilia uzushi na uchonganishi huu unaofanywa kwa makusudi ili kuwachafua viongozi wastaafu,” ameonya Rais Magufuli.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright JAMIIYETU | Designed By BAKI NASI
Back To Top