Jana, Bunge lilitumia zaidi ya saa mbili kupitisha muswada huo huku mvutano ukiibuka katika nyongeza ya mapendekezo ya ununuzi wa dawa na vifaatiba kufanywa kwa dharura na kupinga kwa kamati za fedha na mipango, kuondolewa katika kusimamia mchakato wa zabuni kwenye halmashauri.
Mashambulizi hayo yaliongozwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti, Hawa Ghasia na wabunge Joseph Kakunda (Sikonge), Profesa Anna Tibaijuka (Muleba Kusini) na Andrew Chenge wa Bariadi Magharibi (), kiasi cha kumfanya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), George Masaju kukubali baadhi ya mapendekezo ya Bunge kwa shingo upande.


Post a Comment