Loading...
http://go.ad2up.com/afu.php?id=778977

BREAKING NEWS: SHEIKH PONDA FURAHA YAPOTEA TENA

Sheikh Ponda Issa Ponda, Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania
FURAHA tuliyokuwanayo Watanzania, sasa haipo tena. Ni wakati wa kuhoji, kwanini maisha yamekuwa magumu kiasi hiki?, anaandika Faki Sosi.
Ni kauli ya Sheikh Ponda Issa Ponda, Katibu Mkuu wa Jumuiya na Taaisi za Kiislam Tanzania aliyoitoa leo akizungumza na mwandishi wa habari hii wakati akitoa salamu zake kuelekea Sikukuu ya Eid El Hajj.
Kesho duniani kote, waumini wa Dini ya Kiislam wanatarajia kusherehekea Sikukuu ya Eid el Hajj ikiwa ni sehemu ya ibada kwa mujibu wa imani ya dini hiyo.
Sheikh Ponda amesema, pamoja na kuwepo kwa sherehe hiyo lakini kuna hali ya masikitiko kwa Watanzania kutokana na vipato vya kushukwa jambo ambalo limeonda furaha ndani ya mioyo na familia zao.
Amesema, sikukuu zilizopita katika kipindi kama hiki watu waliweza kutoa sadaka, kulisha masikini, kuchinja kwa ajili ya ibada na kufanya ibada zingine zilizohusisha kipato.
Lakini kutokana na maisha kubadilika, waumini wa dini hiyo wameshindwa kutekeleza yale waliyokuwa wakiweza kuyatekeleza siku za nyuma jambo ambalo linahitaji kutafakari upya mtindo wa maisha ulivyo kwa sasa.
“Tunaelekea kwenye sikukuu lakini jambo ninaloliona kwa sasa ni kwamba, tunapaswa kutafakari upya, kwanini maisha yamekuwa magumu kiasi hiki?
“Siku za nyuma kulikuwa na furaha kubwa hasa wakati wa sikukuu kama huu lakini sasa mambo yamebadilika kwa kiwango kikubwa.
“Watu hawana furaha, maisha yamekuwa magumu. Ni kipindi cha kutafakari kwa mwaka mzima uliopita, tatizo ni nini zaidi?” amesema Sheikh Ponda.
Akizungumzia falsafa ya Hijja Sheikh Ponda amesema, yapo mambo mengi yanayopatikana pale watu wanapotekeleza ibada hiyo.
Amesema, miongoni mwa hayo ni pamoja na kuonesha umoja “kuvaa mavazi ya aina moja, ni kiashirio cha umoja kwamba, pamoja na kuwa watu wanatoka kwenye mataifa mbalimbali, bado wanaunganisha na Uislam.
“Watu wanakutana wakiwa na wadhifa tofauti, mataifa tofauti na uwezo tofauti lakini ndani ya mavazi yake, kila mmoja yupo sawa na mwingine, tunapaswa kuishi maisha ya namna hii,” amesema na kuongeza;
“Falsafa ya kurusha mawe kumpiga shetani ni kiashirio cha kujenga ujasiri katika kukabiliana na yale yote yanayoweza kumyumbisha muumini.”
Hata hivyo amewataka Waislam na Watanzania kwa ujumla kusherehekea sikukuu kwa njia ya amani sambamba na kuchunga miiko na taratibu za dini hiyo popote watakapokuwa.
Akizungumzia tukio la tetemeko lililotokea jana Kanda ya Ziwa (Kagera, Mwanza, Mara, Shinyanga) na kusababisha vifo pia hasara Sheikh Ponda amewapa pole waliofikwa na mkasa huo.
“Nikiwa kama Katibu wa Taasisi na Jumuiya za Kiislam Tanzania, natumia nafasi hii kuwapa pole wale wote waliofikwa na mkaza wa tetemeko la ardhi lililotokea jana Kanda ya Ziwa na nchi jirani.
“Yote yanayotokea yanaletwa na Mungu hivyo hatuna budi kujiandaa kwa kutenda mambo mema ili yatufae kwenye maisha baada ya dunia hii,” amesema.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright JAMIIYETU | Designed By BAKI NASI
Back To Top