Rais John Magufuli leo amemtumbua Mwenyekiti wa Bodi Mamlaka ya Mapato Tanzania, Bernard Mchomvu na kumteua Charles Kichere kuwa Naibu Kamishna Mkuu wa mamlaka hiyo.
Taarifa iliyotolewa asubuhi leo na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa ilieleza kuwa Rais Magufuli ametengua uteuzi wa mwenyekiti huyo na kuivunja bodi hiyo kuwanzia leo.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa mwenyekiti mwingine wa bodi hiyo na wajumbe wake utatangazwa baadaye.
Taarifa nyingine ya mchana iliyotolewa na Ikulu, imeeleza kuwa Rais amemteua Kichere kujaza anajaza nafasi ya Naibu Kamishna Mkuu wa TRA iliyokuwa wazi kwa zaidi ya mwaka mmoja.
Uteuzi huo umeanza mara moja.


Post a Comment