Loading...
http://go.ad2up.com/afu.php?id=778977

Pichaz:..NEWZ..KAMBI KUBWA ZA MAGAIDI ZAVAMIWA NA KIKOSI MAALUM CHA WANAJESHI WA TZ HUKO PWANI

Kikosi maalum cha wapiganaji na majeshi ya ulinzi na usalama kinachopambana na watu wanaojihusisha na ugaidi, wanaosadikiwa kujificha katika mapori ya Mkuranga na Kisarawe Mkoani Pwani, kimebaini uwepo wa kambi kubwa tatu za magenge ya kigaidi katika ukanda wa Pwani ya Tanzania.

Kubaini kwa kambi hizo kumekuja baada ya msako mkali na mapambano ya siku kadhaa yaliyofanywa na wapiganaji hao katika maeneo ya Pwani ambapo wiki iliyopita walifanikiwa kuwatia nguvuni magaidi watano.

Kwa mujibu wa taarifa hizi magenge matatu ya kigaidi yapo katika Mikoa ya Lindi, Morogoro na Pwani katika maeneo ya Kisarawe na Mkuranga ambapo pia kuna idadi kubwa ya wanachama wa magenge hayo.

Taarifa zinazema ni katika ngome hizo ambapo fedha na silaha zinazoporwa na magaidi zinahifadhiwa.

Magenge hayo yana baadhi ya watu ambao ni wazoezi katika medani ya vita na uchunguzi uliofanywa na Taasisi za usalama zimebaini kuwepo na watu zaidi ya 300 waliyojiunga nayo wakiwemo askari wa zamani na kiongozi wao mkuu aliwahi kupata mafunzo ya kikomandoo

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright JAMIIYETU | Designed By BAKI NASI
Back To Top