Kubaini kwa kambi hizo kumekuja baada ya msako mkali na mapambano ya siku kadhaa yaliyofanywa na wapiganaji hao katika maeneo ya Pwani ambapo wiki iliyopita walifanikiwa kuwatia nguvuni magaidi watano.
Kwa mujibu wa taarifa hizi magenge matatu ya kigaidi yapo katika Mikoa ya Lindi, Morogoro na Pwani katika maeneo ya Kisarawe na Mkuranga ambapo pia kuna idadi kubwa ya wanachama wa magenge hayo.
Taarifa zinazema ni katika ngome hizo ambapo fedha na silaha zinazoporwa na magaidi zinahifadhiwa.
Magenge hayo yana baadhi ya watu ambao ni wazoezi katika medani ya vita na uchunguzi uliofanywa na Taasisi za usalama zimebaini kuwepo na watu zaidi ya 300 waliyojiunga nayo wakiwemo askari wa zamani na kiongozi wao mkuu aliwahi kupata mafunzo ya kikomandoo



Post a Comment