Loading...
http://go.ad2up.com/afu.php?id=778977

Virusi vya Zika vyapatikana katika mate na mikojo

Image copyrightEdmar Melo JC Picture
Image captionMtoto aliyeathirika ka virusi vya Zika
Virusi hai vya Zika vyapatikana katika mate na mikojo ya wagonjwa,wanasayansi wa Brazil wamesema.
Matokeo hayo hayamaanishi kwamba ugonjwa huo unaweza kusambazwa kupitia maji maji hayo ya mwilini.Sababu kuu ya kuenea kwa virusi hivyo ni kupitia kuumwa na mbu,lakini wanasayansi wanachunguza njia nyengine.
Huku maambukizi ya Zika yakiwa sio makali,ugonjwa huo umehusishwa na maelfu ya watoto waliozaliwa na kasoro.
Image copyrightEPA
Image captionHarakati za kukabiliana na Zika
Virusi vya Zika pia vimepatikana katika majimaji mengine ya mwilini katika mripuko mwengine uliotokea eneo la Polynesia,lakini mamlaka ya Brazil inasema kuwa hii ni mara ya kwanza virusi hai vya Zika kupatikana.
Paula Gadelha,mkuu wa taasisi ya Fiocruz ambayo inashirikiana na wizara ya Afya amesema:''Virusi hivyo vya Zika vimepatikana katika Mate na mikojo''.
Image copyrightAP
Image captionWanasaynsi wa Brazil
''Lakini hiyo hainamishi kwamba kuna uwezekano wa kuenea kwa virusi hivyo kupitia mate na mikojo.Hatari ya kuenezwa kwa virusi hivyo kupitia maji maji ya mwilini uliangaziwa nchini Marekani ambapo kituo cha udhibiti wa magonjwa kinaamini kisa kimoja kilisambazwa kupitia ngono''.
Hatahivyo kumekuwa na kesi mbili pekee za usambazaji wa virusi hivyo kupitia ngono.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright JAMIIYETU | Designed By BAKI NASI
Back To Top