Loading...
http://go.ad2up.com/afu.php?id=778977

WANACHAMA WAFANYA VURUGU NA KUVAMIA OFISI BAADA YA KURA ZA MAONI CCM KULETA KASHESHE

Baadhi ya vijana wanaosadikiwa kuwa ni wanachama wa chama cha mapinduzi mjini sumbawanga mkoani Rukwa,wamevamia ofisi za chama hicho za wilaya wakishinikiza kutangazwa kwa matokeo ya kura za maoni ya jimbo la sumbawanga mjini,kwa madai kuwa kucheleweshwa huko kuna kila dalili za kuyachakachua matokeo hayo.

Baada ya kufanya vurugu kwa muda kwenye ofisi hizo za wilaya za chama cha mapinduzi mjini sumbawanga,ndipo katibu wa CCM wa wilaya ya Sumbawanga mjini Bw.Gabriel Kiula alipojitokeza na kutangaza matokeo hayo, ambapo amesema aliyeongoza ni mbunge anayemaliza muhula wake mheshimiwa aeshi hilal kwa kupata zaidi ya kura 13,500, na kuwabwaga wagombea wenziwe kumi waliojitokeza mwaka huu.
Kufuatia matangazo hayo baadhi ya vijana wakaibuka na kutaka jina la kiongozi wao huyo lirudishwe bila ya kukatwa, kwa vile ameshinda kwa kishindo, na kutishia kujiondoa kwenye chama, huku mheshimiwa aeshi hilal akiwaomba vijana hao wawe na moyo wa subira na uvumilivu, na kuwashukuru kwa kuonyesha imani kwake.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright JAMIIYETU | Designed By BAKI NASI
Back To Top